Amakuru aryoshye kandi agezweho

banner image

Like US On Facebook

banner image

ZARI aka Lady Boss APEWA ZAWADI YA BAISKELI YA MILIONI 5


Mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Mwandishi wetu

DAKTARI wa Kitengo cha Sayansi na Tiba Asili kilichopo Mbezi-Afrikana, Dokta Fadhili Emily, amemnunulia baiskeli ya kubebea mtoto, mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kama zawadi pindi atakapojifungua.
Mfano wa baiskeli aliyitoa Dkt. Fadhili kwa Zari. Akizungumza na Risasi Mchanganyiko akiwa nchini Sweden alikoenda kwa ziara binafsi, Dokta Fadhili alisema kwa kutambua yeye ni mtu wa Kigoma anakotokea Diamond, ameona amnunulie shemeji yake huyo baiskeli hiyo ambayo kwa mujibu wake, ina thamani ya shilingi milioni 5 za Kitanzania.
Dkt. Fadhili Emily. “Mimi ni mwenyeji wa Kigoma, Zari ni shemeji yangu hivyo nikiwa huku Sweden nimeona niwawakilishe vijana wote wa kule kwa kumnunulia baiskeli hii ya kisasa shemeji yetu, wanatumia wanawake wengi Ulaya kubebea watoto wao,” alisema.
Zari anatarajiwa kujifungua kati ya Agosti au Septemba, mwaka huu ambapo ujio wa mtoto huyo umekuwa ukitengeneza vichwa vya habari kila kukicha.
ZARI aka Lady Boss APEWA ZAWADI YA BAISKELI YA MILIONI 5 ZARI aka Lady Boss  APEWA ZAWADI YA BAISKELI YA MILIONI 5 Reviewed by ibigezwehobyose on Wednesday, June 24, 2015 Rating: 5

Random Post

Powered by Blogger.